Sumu inayotolewa na buibui wa Brazil imekuwa msukumo wa utafiti unaotafuta njia mpya za kutibu saratani.
Kazi hiyo, iliyofanywa karibu miaka 20 iliyopita na wanasayansi kutoka Hospitali ya Israelta Albert Einstein na Instituto Butantan, huko São Paulo, inatathmini uwezo wa kimatibabu wa sumu inayopatikana kutoka kwa Vitalius wacketi, buibui anayeishi pwani ya São Paulo.
Hata hivyo, haijafanywa moja kwa moja kutoka kwa sumu: molekuli zilitengwa, kusafishwa na kuunganishwa katika maabara, kwa kutumia mbinu zilizotengenezwa na wataalam wa Brazil.
Katika utafiti wa awali, molekuli iliyojaribiwa ilionyesha matumaini katika kupambana na leukemia, aina ya uvimbe unaoathiri baadhi ya seli za damu.
Pia iliwasilisha baadhi ya manufaa ikilinganishwa na mbinu zinazopatikana sasa za kutibu ugonjwa huu, kama vile chemotherapy.
Walakini, utafiti wa dutu hii bado iko katika hatua za mwanzo. Ni muhimu kuijaribu kwenye seli zaidi ili kuona usalama na ufanisi – na kisha tu kuanza majaribio na wanadamu.
Wataalamu wanasema tayari wanafanya mazungumzo na makampuni ya dawa ili kuunda ushirikiano na kupata uwekezaji unaohitajika ili kusonga mbele.
Credit; BBC Swahili
#KoncepTvUpdates