Saintfiet amefukuzwa kazi usiku huu,(jana) baada ya kutofautiana sera na uongozi wa
Yanga na sasa Fredy Felix Minziro, aliyekuwa Msaidizi wake, atakaimu nafasi
yake.
Habari zaidi, kuhusu
kufukuzwa kwa kocha huyo, Yanga itatoa taarifa rasmi kesho asubuhi saa 3:00,
makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani.
Mapema leo mchana, uongozi
wa Yanga ya Dar es Salaam, ulitangaza kuisimamisha kazi Sekretarieti nzima ya
klabu, akiwemo Katibu Celestine Mwesigwa na Ofisa Habari, Louis Sendeu,
kutokana na kile ilichoeleza utendaji usioridhisha.
Habari, makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa
Yanga, Clement Sanga alisema kwamba maamuzi hayo yamefuatia kikao cha Kamati ya
Utendaji kilichofanyika tangu saa 5:30 leo hadi saa 9:30.
panga hilo ni Masoud Saad, aliyekuwa Ofisa Utawala, Philip Chifuka aliyekuwa
Mhasibu na Hafidh Saleh aliyekuwa Meneja ambaye anahamishiwa kwenye majukumu
mengine.
sekretarieti nzima, pia tumefanya marekebisho, tumemtoa Meneja wa timu na muda
si mrefu tutamtangaza Meneja mwingie pamoja na sekretarieti mpya,”alisema
Sanga.
Mbelgiji, Tom Saintfieti anapewa onyo kali kwa kuzungumza ovyo na vyombo vya
habari.
“Tumekwishakutana naye mara
kadhaa kumpa utaratibu wa kuzungumza na vyombo vya habari, sasa tutamuandikia
barua ya kumkumbusha wajibu wake na kuzingatia wajibu wake, kutozungumza na
vyombo vya habari holela,”alisema.
yanakuja baada ya Yanga kuanza vibaya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara,
ikiambulia pointi moja tu katika mechi zake mbili za awali, kutokana na sare ya
bila kufungana na Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya Jumamosi na
Jumatano ikachapwa mabao 3-0 Morogoro Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Yanga na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Lawrence Mwalusako atakaimu
nafasi ya Katibu wa klabu hiyo, kufuatia kusimamishwa kwa Celestine Mwesigwa,
wakati kiungo wa zamani wa klabu hiyo, Sekilojo Johnson Chambua atakuwa Meneja
mpya wa klabu hiyo, akirithi mikoba ya Hafidh Saleh.
Habari kutoka ndani ya
Yanga, zimesema kwamba viongozi hao wapya watatangazwa wakati wowote kuanzia
sasa kurithi nafasi za viongozi walioondolewa madarakani, kutokana na kile
kilichoelezwa utendaji usioridhisha.
mpya, iliyoachwa wazi na Philip Chifuka itakuwa chini ya dada mmoja, aliyetajwa
kwa jina moja tu, Rose aliyekuwa akifanya kazi ofisi hiyo kwa muda mrefu,
wakati Msemaji wa klabu iliyoachwa wazi na Louis Sendeu, inaelezwa atapewa
mdogo wa mke wa Ridhiwani Kikwete, aliyehesabu kura za Abdallah Bin Kleb katika
uchaguzi mdogo wa klabu, Julai 14.